Quantcast
Channel: AutomobileHeat » css
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1303

Baraza Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa Lamaliza Mikutano yake kwa Kishindo.

$
0
0

Rais wa Baraza Kuu la 69 la Umoja wa Mataifa, Bw. Sam Kutesa akigonga nyundo maalum kuashiria kukamilika kwa Mikutano ya Baraza hilo ambalo ameliongoza kwa mwaka  mzima. Kushoto kwake  ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akiwa mwenye furaha wakati wa kuhitimishwa  Baraza la 69 ambapo alimpongeza Bw. Sam Kutesa kwa kuliongoza  Baraza kwa uhodari  uliopelekea kupitishwa kwa maazimio mbalimbali. Na MwandishiMaaalum New York Mkutano wa  69 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,   uliokuwa chini  ya Urais wa  Waziri wa Mambo ya Nje wa  Uganda Bw, Sam Kutesa umefikia ukingoni siku ya jumatatu  kwa kupitisha maamuzi ya kihistoria ambayo pamoja na  mambo mengine yanatoa mwelekeo wa majadiliano kuhusu  marekebisho na mageuzi ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja  wa Mataifa. Maamuzi hayo ambayo kwa mara ya kwanza yanaingizwa  rasmi katika nyaraka muhimu za Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa na yaliyopewa namba A/69/L.92 yalipitishwa kwa  kauli moja na wajumbe kutoka nchi 193 wanaounda Baraza  Kuu la Umoja wa Mataifa. Maamuzi hayo ambayo baadhi ya wazungumzaji  waliyapachika jina kama maamuzi ya Kutesa ikiwa ni ishara  ya kutambua mchango wake katika kusimamia kidete  majadiliano kuhusu mageuzi ya Baraza Kuu la Usalama la  Umoja wa Mataifa yanatoa msingi  au maandishi ambayo  yatawawezesha Nchi Wanachama kujadiliana kwa kupitia  maamuzi hayo. Ingawa maamuzi hayo yamepita bila  kupigiwa kura na  kupongezwa kwa kufungua ukursa mpya katika kuendeleza  mchakato wa majadiliano ya mageuzi na upanuzi wa Baraza  Kuu la Usalama,  baadhi ya nchi zimeyaelezea maamuzi hayo  kuwa ni ya kiufundi zaidi na hivyo yasikuchukuliwe kama  maamuzi ya mwisho kwa madai kwamba, maandalizi na  majadiliano ya maamuzi hiyo hayakuwajumuisha na hivyo  hayawakilishi nina hisia za makundi yote. Akiungana na wazungumzaji wengi waliounga mkono  kupitishwa kwa maamuzi hayo Mwakilishi wa Kudumu wa  Tanzania katika Umoja wa Mataifa,   Balozi  Tuvako Manoni, amesema ,majadiliano yaliyopelekea  kupatikana kwa maamuzi hayo hayakuwarahisi, lakini  yameasisi hatua mpya ya mwendelezo wa ajenda ya  kulifanyia mageuzi Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa  Mataifa ili liwejumuishi kuendana na mazingira ya sasa. Akasema hapana shaka kwamba majadiliano   Zaidi  yanapaswa kuendelea ili kujibu kiu ya kila upande na  kwamba nchi wanachama wanapaswa kujivunia hatua  hiyo muhimu hata kama ni hatua ndogo. Akatumia fursa hiyo kuwapongeza Bw.Sam Kutesa na  Mwakilishi wa kudumu wa Jamaica Balozi Rattray kwa kazi  nzuri , kubwa na iliyokuwa na changamoto nyingi lakini  iliyofanikisha kupatika kwa maamuzi hiyo. Majadiliano kuhusu namna ya kuboresha na kupanua  wigo wa wajumbe wa Baraza Kuu la  Usalama la Umoja  wa Mataifa, ni majadiliano yaliyoaza mwaka 2008 lakini  ni katika Mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la Umoja wa  Mataifa ambapo matokeo ya majadiliano miongoni mwa  wanachama yameweza kupitishwa rasmi katika Baraza  Kuu la  Umoja wa Mataifa. Muundo wa sasa wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja  wa Mataifa ambalo lina wajumbe wakudumu na wenye  kura ya turufu watanona wajumbe  10 wanaoingia kwa  mzunguko wa uwakilishi wakiandaa haujaitendea haki  Afrika  bara ambalo lilokumbwa kwa asilimia kubwa ya  maamuzi yanayofanywa na Baraza Kuu la  Usalama  yanaihusu Afrika lakini Afrika si mwanachama wa  kudumu na hiyvo imekuwa ikipigania kupata nafasi ya  uwakilishi wa kudumu pamoja na kura ya turufu. Kumalizika kwa Mkutano wa 69 wa Baraza Kuu la   Umoja wa Mataifa,  kunafungua kuanza kwa Mkutano  wa Baraza Kuu la 70 ambalo kwa mwaka mzima  litakuwa chini ya Urais wa Bw.Monges Lykketoft.

[via LEKULE]

Follow us @automobileheat – lists / @sectorheat


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1303

Trending Articles